Tuesday, October 30, 2012

UJENZI WA LANGO (GETI) KUU LA SHULE SHULE YA MSINGI KALOLENI

Shule ya Msingi Kaloleni kupitia ushirikiano na Chrysalis School ilianza ujenzi wa uzio wa shule kwa kujenga fensi mwaka 2009. Kazi iliyobakia ni kuweka geti na ujio wa wageni hao umewezesha shule kuwa na geti sasa. Kwa sasa wanafunzi wanasoma katika mazingira mazuri kama inavyoonekana hapa:

JIKO LA SHULE LABORESHWA

Kupitia juhudi za kimashirikiano kati ya Shule hizi mbili, jiko la shule limeboreshwa. Kwa sasa Mpishi wa shule anapikia katika mazingira mazuri; jengo limeboreshwa, mfumo wa maji umeingizwa jikoni na jiko limeboreshwa kabisa.
Ujenzi ulianza mwezi wa Juni na umekamilika mwezi wa October. Ona jinsi ambavyo kazi hizi zimefanyika:

SHULE YA MSINGI KALOLENI YABORESHA OFISI NA JIKO

Shule ya Msingi Kaloleni kwa mwaka huu wa 2012 imeweza kuboresha Ofisi ya waalimu, Ofisi ya Mwalimu Mkuu pamoja na kulifanyia matengenezo jiko la shule. Hii imewezekana kupitia ushirikiano ulioanza miaka mitatu iliyopita kati ya shule hii na shule moja katika jimbo la Montana huko Marekani. Wageni hawa walifika Kaloleni mwezi wa Juni na kushirikiana na wanakaloleni kufanya yote haya.


Friday, October 15, 2010

NAIBU KATIBU MKUU ALIPOTEMBELEA WAKULIMA MPUNGA KALOLENI

Naibu Katibu Mkuu - Tamisemi alipotembelea ujenzi wa mifereji ya umwagiliaji Kaloleni

Naibu Katibu Mkuu - Tamisemi akiwa pamoja na Maafisa Kilimo, wahandisi pamoja na wakulima akisisitiza jambo katika chanzo cha mfereji wa Njoro ya Liwali.
Mkaguzi wa Ndani Manispaa ya Moshi alipotembelea mradi wa ujenzi wa mifereji kwa ukaguzi pamona na maafisa Kilimo akihoji mambo mkulima mmoja ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Usimamizi wa Mifereji wakati wa ujenzi wa mfereji Njoro ya Liwali katika Msitu wa Njoro.



MRADI WA KUJENGA TANKI LA KUHIFADHI MAJI SHULE YA MSING KALOLENI WAANZA

Ujenzi wa Kisima tanki la maji kusaidia uhifadhi wa maji safi kwa shule
Fundi akiwajibika kujenga mahali ambapo tanki la maji safi litawekwa na kuondokana na tatizo la uhifadhi wa maji usio na tija kama wanavyoonekana wanafunzi wakichota maji kwenye kisima kilichopo shuleni ambacho hakina uwezo kuhifadhi maji mengi na kwa usalama.


UJENZI WA UZIO SHULE YA MSINGI KALOLENI KARIBU KUKAMILIKA

Ujenzi wa uzio kaloleni shule ya Msingi umefikia karibu kukamilika. Wiki hii 98% shule imezungushiwa uzio. Haya ni mafanikio ya kipindi kifupi tu cha mwaka mmoja uliopita. Pichani juu, uzio ukiwa umekutanika na uzio wa Shule ya sekondari Msasani.
Angalia uzio wa shule ya msingi Kaloleni eneo jirani na shule ya sekondari Msasani.


Saturday, May 15, 2010

WANANCHI KWENYE MKUTANO SERIKALI YA MTAA

Mzee mmoja akiteta jambo
Akina mama nao hawako nyuma

vijana nao wamo