Thursday, December 17, 2009

UJENZI WA MADARASA MSASANI SEKONDARI - KALOLENI WAENDELEA

Chumba kimoja cha darasa kimefikia hatua hii, hapa mafundi wanachakarika
Vyumba vingine vitatu vipo hatua ya msingi.

Mhandisi wa Manispaa ya Moshi akikagua ubora wa kazi.


Ubora wa kazi nimuhimu.




Mhandisi akiangalia nondo zilivyosukwa kabla ya kuruhusu kazi kuendelea.




WAJUMBE WA WDC BAADA YA UKAGUZI ZAHANATI


Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi akiwaongoza wajumbe kurejea Kikaoni baada ya wajumbe wa WDC Kaloleni kujionea maendeleo ya Kazi ya Ujenzi wa zahanati ya TASAF Kata Ya Kaloleni.

WDC YA KUFUNGA MWAKA YAKUTANA JANA

WAJUMBE WAKIMSIKILIZA MWENYEKITI (hayupo pichani)

Kikao kiliamia katika zahanati ya Kata kuona maendeleo ya kazi. Hapa Mwenyekiti wa kamati ya Ujene akiwaongoza wajumbe kuona kazi ilipofikia
Wajumbe wa WDC wakifuatilia maelezo ya Mwenyekiti wa kamati ya Ujenzi zahanati.


Meza Kuu, Katibu akitoa maelezo kwa wajumbe huku Mwenyekiti akifuatilia kwa karibu.




Tuesday, December 15, 2009

UJENZI WA ZAHANATI WAFIKIA PLASTA

Mafundi wakimalizia hatua ya plasta
Mafundi kazini plasta


Kazi ya kuchanganya zege


Monday, December 14, 2009

HALI YA UJENZI WA ZAHANATI YA KATA KALOLENI MWEZI WA NOVEMBER

sehemu ya nje
Kwa ndani tayari plasta imewekwa


Kwa ndani kulivyo


Friday, October 30, 2009

Wednesday, September 16, 2009

Kikao cha Mtaa
Wakulima na diwani wao

Wakulima na diwani wao



Zahanati ikipauliwa



MAMBO YA KALOLENI

Mkutano wa Mtaa wa Kaloleni, chini ya Mwenyekiti wa Mtaa, Mzee Maulidi
Hawa ndio askari Kata ambao wanajaribu kuboresha hali Kaloleni


Tuesday, September 1, 2009

MAENDELEO YA UJENZI WA ZAHANATI

Zahanati ya Kata ya Kaloleni ikiwekwa fremu za madirisha.

Mh. Diwani akikagua ndani ya nyumba mpya ya walimu Msasani Secondari. Mbele ni mwandishi wa habari radio Free Africa Mwanza.

DIWANI NA WENYEVITI WA MITAA WATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO KALOLENI


Mh. Diwani Michael Mwita akiwa na Kaimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Msasani wakikagua nyumba mpya ya walimu ambayo iko katika hatua za mwisho kwa ajili ya makazi ya walimu shuleni.

Saturday, August 29, 2009

MKUTANO WA HADHARA WA MTAA KALOLENI - KALIMANI

AUGUST ILIVYOKUWA KALOLENI

Katika kufunga wikiendi ya mwezi wa august, Katika Kata ya Kaloleni yamefanyika mambo mengi sana. Hebu jionee mwenyewe.

Sunday, August 2, 2009

MATUKIO KALOLENI JULY

Baada ya siku kadhaa ilifikia siku ya wageni kuondoka Kaloleni. Hapa Mr. Kenny akihutubia katika tafrija fupi iliyofanyika.
Wageni pamoja na walimu wa Kaloleni katika picha ya ukumbusho.

Afisa Mtendaji wa Kaloleni(miwani) katika kikao na wakulima wa mpunga wa Kaloleni, hapa wakijadiliana jambo.



Wakuu wa shule wawili wakijadiliana siku ya mwisho ya ziara ya wageni kutoka Marekani. Hapa ni Madam Marry wa Chrysalis School na Bi. Chuo wa Kaloleni Primary.



WAMAREKANI WAKIFANYA KAZI KALOLENI

Walimu wa Shule ya Msingi Kaloleni wakiwajibika pamoja na wageni

Kazi ya ukarabati ya darasa ilipokwisha, Madam Marry(Headmistress Chrysalis School, mwenye kamera akiwa na mratibu wa ziara ya wageni hao Madam Kate) wakifurahia darasa lililokarabatiwa.

Mkuu wa shule Chrysalis High School akiwa bize katika ukarabati wa darasa mojawapo.

Walimu wakisaidiana na mmoja wa wamiliki wa Shule hiyo, Mr. Kenny katika ukarabati wa sakafu darasa la kwanza.
Kata ya Kaloleni mwezi uliopita ilipata ugeni wa kikundi cha wanafunzi na walimu wao wapatao 13 kutoka Chrysalis High School nchini Marekani. Wageni hawa waliitembelea shule ya Msingi Kaloleni na kukaa kwa siku tano wakifanya kazi za kujitolea katika kuiboresha shule hiyo.









Sunday, July 19, 2009

KALOLENI ILIPOTEMBELEWA NA WAGENI KUTOKA MAREKANI



Wanafunzi kutoka Chrysalis High School katika Jimbo la Montana wakiwa katika harakati za kubeba mchanga shughuli za ujenzi walizofanya.


Kazi na furaha, wanafunzi kutoka Marekani wakiwa wamebebana kwenye toroli kuchukua kokoto.


Bi. Kate wa Mondo Challenge (mwenye sketi nyekundu) ambaye alikuwa mratibu wa ziara hii akiwa na wanafunzi hao muda mfupi kabla hawajaanza kukoroga zege katika kazi ya ujenzi wa uzio wa shule ya Msingi Kaloleni kama inavyoonekana.
















Afisa Mtendaji wa Kata kama kiungo kikuu cha wageni hawa alijumuika nao katika kazi kila siku. Hapa pamoja na wanafunzi wawili kabla ya kazi kuanza.

Monday, May 25, 2009

MKUTANO WA ULINZI MSASANI ULIVYOKUWA

Wananchi wakifuatilia majadiliano ya kikao
Mjumbe Bw. Temba akiteta jambo na wananchi wenzake kidemokrasia


Mwananchi akiomba nafasi ya kuchangia


Akina mama nao walikuwepo; hapa wakiwa makini wakifuatilia yanayosemwa.



Kata ya Kaloleni iko katika hatua za awali za kuimarisha ulinzi wa sungusungu katika mitaa yake ya Kalimani na Kaloleni. Pia wananchi wa eneo la Msasani katika Mtaa wa Kaloleni wameamua kuanzisha juhudi hizo kwa kupanga mikakati ya kuanzisha doria ya sungusungu. Katika kikao chao na uongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Kata, wananchi hao waliwapigia kura watu wanaowatuhumu kuwa ni waizi na wahalifu wa aina mbalimbali kama picha zinavyojionesha hapo juu.









KITONGOJI CHA MSASANI CHAFANYA KIKAO CHA ULINZI

Wananchi wakiwasikiliza viongozi
Mjumbe akichangia hoja ya kudumisha ulinzi


Baadhi ya vijana watakaofanya shughuli za ulinzi "sungusungu" wakiwa wametoka mbele

Mheshimiwa Diwani wa Kata ya Kaloleni akiwahutubia wananchi. Waliokaa ni wenyeviti wa Mitaa na Afisa Mtendaji wa Kata. Hii ilikuwa katika kikao cha Kamati ya Ulinzi kilichofanyika tarehe 17/5/2009 kwa Mzee Tondi kuzungumzia kuibuka kwa matukio ya wizi katika eneo la Msasani.




Thursday, March 5, 2009

RC BABU WA KILIMANJARO AITEMBELEA KATA YA KALOLENI


Hapa Mh. Babu akielezwa maendeleo ya ujenzi na Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi , bw Gasper Mkuji huku Mkuu wa Shule akiangalia.

Mkuu wa shule akitoa maelezo kwa wageni waheshimiwa

RC. Babu akitoa hotuba fupi juu ya ziara yake Shuleni Msasani Secondari.
Aliyekaa kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa Bernadete Kinabo.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro alitembelea Kata ya Kaloleni mapema wiki hii ambapo alikuja kukagua miradi ya Maendeleo hasa shule ya sekondari Msasani na Mradi wa ujenzi wa Mfereji wa Njoro ya Goa.
Katika ziara hiyo, aliongozana na Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Mh. Musa Samizi na Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi, Bernadette Kinabo pamoja na wakuu wa idara mbalimbali za Manispaa na maafisa kadhaa kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.